...

Kikaratasi cha maswali

Wito wa kuchangia: Utafiti kuhusu kuandaa Mpango Mkakati wa Mahakama ya Afrika mwaka 2026-2028

Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ina jukumu muhimu katika kulinda haki za binadamu barani Afrika. Kwa kutoa maamuzi zaidi ya 400, imeonyesha busara kubwa ya kisheria kuhusu masuala muhimu kama vile kulinda jamii za wazawa, haki za mazingira, uadilifu wa uchaguzi, uhuru wa kujieleza na haki ya kusikilizwa kwa haki. Ushawishi wake umeenea hadi kwenye mifumo ya kisheria ya kitaifa, ambapo maamuzi muhimu yametajwa na mahakama za ndani na kuhamasisha kutungwa sheria mpya za haki za binadamu katika Nchi mbalimbali Wanachama wa Umoja wa Afrika.

Mahakama ya Afrika inapoandaa Mpango Mkakati wake wa mwaka 2026-2028, utaalamu wako ni muhimu. Utafiti huu unalenga kupata mtazamo wako kuhusu vipaumbele vyake vya baadaye ili kuimarisha michakato yake, juhudi za kuifikia jamii na ufanisi wa jumla. Tunakuhimiza ushiriki na kusaidia kuunda Mahakama ya Afrika inayofikika zaidi na yenye matokeo, ikijumuisha kweli "Suluhu za Afrika kwa Matatizo ya Afrika".

01 Jina na Mawasiliano (Hiari)
Jaza tu kama « zingie » zimeshachaguliwa
Tafadhali andika kwa ufupi kadiri iwezekanavyo katika majibu yako. Unakaribishwa kujibu maswali ambayo upo huru kujibu au uliyo na uelewa mahususi kuyahusu.

Kikaratasi cha maswali


Kwa nini unaamini hivi vinapaswa kuwa vipaumbele vya juu?
03 Mahakama inawezaje kuboresha michakato yake ya mahakama ili iwe na ufanisi zaidi katika kulinda haki za binadamu barani Afrika?
Ni kwa njia gani Mahakama inaweza kuongeza uelewa kwa watu kuhusu mamlaka na busara zake za kisheria?
Mahakama inawezaje kushughulikia changamoto hizi?
Mahakama inawezaje kuiga au kuendeleza mafanikio/mbinu bora hizi?
Hii inaweza kuhusishwa na maeneo mapya makuu, teknolojia, ushirikiano au mageuzi ya kiutaratibu.

Dira, Damira na Maadali ya Msingi ya sasa kwa ajili ya rejea:

Dira: "Afrika yenye utamaduni wa kudumu wa haki za binadamu."

Dhamira: "Kukamilisha mamlaka ya ulinzi ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kwa kuimarisha mfumo wa ulinzi wa haki za binadamu barani Afrika na kuhakikisha Mkataba wa Afrika unaheshimiwa na kuzingatiwa, pamoja na mikataba mingine ya kimataifa ya haki za binadamu, kupitia kazi zake za kimahakama."

Maadili ya Msingi:

  1. Uhuru wa mahakama na kutopendelea upande wowote kati ya wahusika wa kesi na wadau.
  2. Matumizi ya haki na yasiyo na upendeleo na tafsiri ya vifungu vya Mkataba wa Afrika, mikataba mingine muhimu ya kimataifa ya haki za binadamu, Itifaki na Kanuni.
  3. Uwazi na uwajibikaji wa kimaadili katika shughuli zote za Mahakama.
  4. Kutetea uhuru wa kila mtu kufurahia haki za msingi za kiraia, kisiasa, kijamii, kiuchumi na kitamaduni.
  5. Ushirikiano na wadau husika katika kufanikisha lengo la Mahakama la kulinda haki za binadamu na watu.
  6. Kutobagua na kuwa na usawa katika utendaji wa kazi ya Mahakama.
  7. Uadilifu wa Majaji na wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye Mahakama.
  8. Kutoa fursa sawa kwa watumiaji wote watarajiwa wa Mahakama.
  9. Kushughulikia kwa haraka mahitaji ya wale wanaoifikia Mahakama.

Asante kwa muda wako na kujitoa kwako kuhakikisha haki za binadamu barani Afrika!